
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amewashauri viongozi wazee na waliokaa madarakani muda mrefu kuacha kung’ang’ania madaraka.
Aliongeza: “Haiwezekani mzee ukakaa kundi moja na kijana wako
 aliyetahiriwa juzi, kwani kwa kawaida, kijana akitahiriwa hupandishwa 
daraja na kukaa kundi la wakubwa, hapo wewe baba yake hata kama una 
miaka 40, unahamishwa na kuingia kundi la wazee.”

Januari 14, 2010, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, aliwashauri wazee 
watumie busara kupima uamuzi wa kugombea tena nafasi za ubunge kwenye 
uchaguzi mkuu. Pinda alitoa rai hiyo alipokuwa akijibu maswali ya 
wahariri katika mkutano alioitisha kujibu maswali yao jijini Dar es 
Salaam.
Warioba alisema mtazamo wake ni vyema kuwa na ukomo wa mtu kuwa mbunge, ambapo alipendekeza vipindi vitatu vya miaka mitano mitano yaani miaka 15
 
 
 
No comments:
Post a Comment