Pages
Home
Kitaifa
Kimataifa
Michezo
Burudani
Makala
Usilolijua
Leo katika historia
Picha
Teknolojia
Afya
Simplfy language
thanx
Sunday, June 29, 2014
AJABU:AKABIDHI SHANGA ZA MAJINI KANISANI...
Mwanamke anayefahamika kwa jina la Asnath Terevaeli akikabidhi shanga kwa Mchungaji Kiongozi, (Frank Endrew) wa Kanisa la Ufufuo na Uzima mkoani Arusha.
Katika hali ya kushangaza, mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Asnath Terevaeli hivi karibuni aliamua kukabidhi kanisani shanga za majini kwa kile alichodai kuwa, zimekuwa zikimtesa na kumfanya akose amani.
Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita katika Kanisa la Ufufuo na Uzima mkoani hapa baada ya moto wa Injili kuwashwa na Mchungaji Kiongozi, Frank Endrew.
Akizungumza na Risasi Jumamosi, mmoja wa waumini wanaosali kanisani hapo aliyejitambulisha kwa jina la Yusta John alisema, awali mwanamke huyo alionekana mwenye jambo linalomtatiza na lilipotolewa tangazo la wenye matatizo kupita mbele, Asnath alifanya hivyo huku akiwa ameshika shanga mkononi.
“Watu wengi walikuwa na shauku ya kujua lililomsibu mama huyo lakini alipofika alimkabidhi mchungaji Frank shanga hizo zilizotengenezwa kiasili zinazodaiwa ni za majini.
Shanga zilizosalimishwa.
“Mwenyewe alieleza kuwa, alipewa kama zawadi na mwanaye lakini cha ajabu zimekuwa zikimtesa na kumfanya akose amani.
Mchungaji Gwajima
“Alidai kuwa kila alipovaa alihisi mauzauza mwilini hivyo akaona sehemu sahihi ya kujikomboa na mateso hayo ni kanisani,”
alisema Yusta.
No comments:
Post a Comment
Newer Post
Older Post
Home
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment