Watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wamemuua kinyama kwa kupiga risasi moja ya kichwani mwenyekiti wa chama cha mapinduzi kata ya Busambala wilayani Butiama mkoani Mara Bw Willison Opio mwenye umri wa miaka 60 huku kichwa chake kikisambaratishwa kabisa na risasi hiyo.
Mauaji hayo ya kinyama yamefanyika saa saba usiku wa kuamkia jana,baada ya majambazi hayo kuvunja milango ya nyumba aliyokuwa amelala kiongozi huyo na familia yake katika kijiji cha Kwikuba kabla ya kumshambulia kwa bapa za panga mke wamarehemu Bi Agness Wambura ambaye alilazimika kuwapa kiasi cha shilingi laki nne ambazo alizikopa kutoka katika taasisi moja ya fedha.
No comments:
Post a Comment