
MKALI wa vichekesho Bongo, Haji Salum ‘Mboto’ 
ameibuka na kusema kuwa endapo atafariki dunia mwili wake ukaagiwe 
katika Viwanja vya TCC Chang’ombe na siyo Leaders kama ambavyo imekuwa 
ikifanyika kwa wasanii wengi wanapokufa.
Akizungumza na paparazi wetu kwenye Viwanja vya Leaders
 wakati wa msiba wa msanii mwenzake, achel Haule ‘Recho’, Mboto alisema 
tayari ameshaacha wosia kwa marafiki zake kwamba siku akifariki dunia 
mwili wake uagiwe TCC kwani yeye nyumbani kwao ni Temeke na ndugu zake 
wengi wapo huko na endapo wosia huo utakiukwa jeneza lake litagoma 
kubebeka.
“Mimi nimeshawaambia marafiki zangu kwamba siku nikifa 
mwili wangu uagiwe TCC Chang’ombe kwa sababu ndiyo nyumbani kwetu, 
naomba wale niliowaambia walizingatie hilo wakiona linakiukwa wagome na 
jeneza langu ligome kubebeka,” alisema Mboto
 
 
 
No comments:
Post a Comment