Akizungumza kwa uchungu na gazeti hili akiwa wodini kwenye Hospitali ya Mkoa wa Kitabibu Kinondoni, Mwananyamala jijini Dar, Yusta ambaye amefanya kazi kwa tajiri yake huyo kwa miaka mitatu alisema:
“Kwanza nataka watu wajue kuwa mwajiri wangu ni binamu yangu, alinileta hapa Dar kwa ajili ya kumsaidia kazi za ndani pamoja na kumlelea mwanaye.
“Kipigo hasa kilianza mwanzoni mwa mwaka huu ikiwa ni pamoja na kuning’ata kwa meno mwili mzima, ndiyo maana mwili wangu wote unaonekana una mabakamabaka.
“Mateso yangu majirani walikuwa wakiyajua kutokana na kilio changu lakini walikuwa wanashindwa kunisaidia kwa sababu ya ushirikiano mdogo.
No comments:
Post a Comment