Simplfy language

thanx

Monday, June 2, 2014

MAONO KABLA YA KIFO CHA MSANII RECHO

Saguda akiwa na siamanzi baada ya kuondokewa na mkewe Recho Haule.
KOMEDIAN mahiri Bongo, Haji Salum ‘Mboto’ amefunguka kuwa Saguda alikijua kifo cha mpenzi wake, Sheila Haule ‘Recho’ kutokana na kauli zake alizokuwa akimwambia pindi alipokuwa akimuomba acheze filamu na mkewe kisha akafariki kabla haijatoka.

Akizungumza katika mahojiano maalum aliyofanya na paparazi wa Global TV Online (inapatikana kupitia
, Mboto alisema kuwa wakati Recho anakaribia kujifungua, Saguda alimfuata na kumuomba amsaidie kucheza naye filamu lakini akakataa.

“Saguda alinibembeleza sana mwisho wa siku akaniambia Mboto huwezi jua nini Mungu amekipanga mbele, kubali kucheza na mke wangu, kiukweli nilikubali kwa shingo upande na nikawa nacheza nje ya mudi kutokana na kwamba sikuipenda ile hali ya Recho kwa kuwa niliogopa tunaweza kubishana au kugombana na yeye ni mjamzito, maskini kumbe ndiyo ilikuwa filamu yake ya mwisho,” alisema Mboto huku akibubujikwa na machozi.

Kwa mujibu wa Mboto, hiyo ilikuwa ni filamu ya tatu kushiriki na wahusika wakuu kufariki dunia. Ya kwanza ni Kijiji cha Tambua Haki (Steven Kanumba), The Boss (Adam Kuambiana) na hiyo ya mwisho itakayojulikana kwa jina la Fedheha

No comments:

Post a Comment