MAHABUSU wawili kati ya sita wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji,
wameleta kizaazaa baada ya kujaribu kutoroka na kukimbilia kwenye
mlingoti wa Bendera ya Taifa nakuing’ang’ania kisha kuvua nguo na mmoja
wao kubaki mtupu.
Tukio hilo limetokea leo majira
ya saa 4:00 asubuhi katika Mahakama ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya
Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, wakati mahabusu hao walipofikishwa
kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi zao, lakini ghafla walipofika kwenye
viwanja vya mahakama hiyo walitimua mbiyo kuelekea kwenye mlingoti wa
Bendera hiyo ya Taifa na kuvua nguo.
Inspector
Henry akiwasihi mahabusu hao wawili wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji,
kuachia mlingoti wa Bendera ya Taifa na kurudi kwenye chumba cha
mahakama kwaajiri ya taratibu za kesi.
Askari polisi wakiwalinda mahabusu wawili kati ya sita wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji
Inspector
Henry (shati la bahari) akiwa na Inspector Veda (mwenye koti)
wakisikiliza hoja za Thobiasi Warioba (35), aliyeamua kuvua nguo zote na
kubaki mtupu akiwa ameng’ang’ania mlingoti wa Bendera ya Taifa
Ushawishi ukiendelea.
Mahabusu
Thobiasi Warioba (aliye mtupu) pamoja na mwenzake Hamis Ramadhani katu
katu waking’ang’ania mlingoti wa bendera ya Taifa huku wakishinikiza
kuzungumza na waandishi wa Habari.
Wananchi wakiwa wamefurika viwanja vya mahakama.
Baada ya kuzungumza na waandishi wa habari mahabusu hao walikubali kurejea chumba cha Mahakama.
Nje ya Mahakama kuelekea lango kuu.
Wananchi wamefurika viwanja vya mahakama.
“Haiwezekani, tangu mwaka 2011 tulipokamatwa hadi sasa kesi zetu
hazijasikilizwa. Wengine tumebambikiziwa kesi. “Tunaomba haki zetu,
polisi mnatuonea, vyombo vya habari tunaomba mtusaidie tumekaa muda
mrefu bila kusikilizwa na hatujui hatma yetu tangu 2011 tulipo kamatwa
tumechoka kukaa mahabusu, tunaomba kesi zetu zisikilizwe”.
No comments:
Post a Comment