Akizungumza na gazeti hili, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, alisema nyumba hiyo ilivamiwa Januari 11 kati ya saa 8 usiku na alfajiri.
“Kuna kijana walimhisi kufanya wizi huo ambaye alikuwa akifanya kazi hapo kwa karibu miaka miwili lakini alifukuzwa kutokana na tabia ya udokozi, siku mbili kabla ya wizi huo alionekana hapo na alipoondoka wizi huo ukafanyika,” alisema Kamanda Wambura na kuongeza kuwa kuna mtuhumiwa mwingine anatafutwa
No comments:
Post a Comment