Pages
Home
Kitaifa
Kimataifa
Michezo
Burudani
Makala
Usilolijua
Leo katika historia
Picha
Teknolojia
Afya
Simplfy language
thanx
Wednesday, January 15, 2014
Hofu ya hali kuzorota nchini..............
Hofu
ya hali kuzorota..............
CAR
Licha ya tahadhari ya UN, watu mjini Bangui walikuwa na furaha baada ya Rais wa mpito Michel Djotodia kuondoka mamlakani
Mjumbe wa ngazi ya juu katika Umoja wa Mataifa ametoa wito kwa jamii ya kimataifa kufanya juhudi zaidi kuisaidia Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Akiongea na BBC mjini Bangui, John Ging alisema kuwa nchi hiyo iko kwenye mzozo mkubwa unaohitaji kutatuliwa.
Bwana Ging amesema watu wengi bado wanaishi kwa hofu ya mashambulizi ya kidini na kikabila.
Kadhalika alisema kuwa wasiwasi mkubwa kwa sasa hivi ni kuwa hali huenda ikazorota zaidi
.
Wiki jana,Umoja wa mataifa ulionya kuwa nchi hiyo inakabiliwa na mzozo mkubwa wa kibinadamu kwa sababu watu wameanza kutoroka vita na kutafuta hifadhi katika kambi za muda.
Ameeleza kuwa kambi hizo hazina huduma muhimu na kuwa mazingira ni chafu.
Tayari kumekuwa na mlipuko wa Ugonjwa wa Surua katika uwanja wa ndege wa Bangui ambako watu 100,000 wamepata hifadhi .
Mjumbe huyo amesema kuwa idadi kubwa ya watu walioachwa bila makao,ni dalili ya kutosha kuwa mamilioni ya watu wamelazimika kutoroka makwao.
No comments:
Post a Comment
Newer Post
Older Post
Home
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment