Pages
Home
Kitaifa
Kimataifa
Michezo
Burudani
Makala
Usilolijua
Leo katika historia
Picha
Teknolojia
Afya
Simplfy language
thanx
Wednesday, October 16, 2013
Waumini wa dini ya Kiislam wamejitokeza kuhudhuria ibada ya swala ya Eid el Hajj.
Waumini wa dini ya Kiislam wamejitokeza kuhudhuria ibada ya swala ya Eid el Hajj.
Mamia ya waumini wa dini ya kiislamu wamejitokeza kuhudhuria ibada ya swala ya Eid el hajj zilizofanyika kitaifa katika makao makuu ya baraza kuu la waislamu Tanzania-Bakwata kinondoni jijini Dar es Salaam.
Ibada hiyo ya sikukuu ya Eid al hajj iliyofanyika katika masjid Farouk Kinondoni jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na mgeni rasmi waziri wa maji Mh Profesa Jumanne Maghembe pamoja na viongozi mbalimbali na waumini wa dini ya kiislamu katika ibada hiyo.
Ibada hiyo iliendana na kusomwa kwa Quruan tukufu mabapo ustaadh Abdul Jabar alipata nafasi ya kusoma Quruan tukufu na kisha sheikh wa wilaya ya Kinondoni shekh Ahmed Mohamed Muhenga alihubiri akisema ni vyema waumini wa dini ya kiislamu kote nchini kuishi kwa kupenda amani kwani mwenyezi Mungu ana tabia ya amani.
Katibu mkuu wa Bakwata Suleman Lolila,akitoa salaam kwa niaba ya Bakwata kwa mgeni rasmi Mh profesa Jumanne Maghembe,alianza kwa kupongeza hatua nzuri iliyofikiwa na serikali kwa kuandaa mchakato wa katiba mpya huku kaimu mufti sheikh Habib Ismael Makusanya akisisitiza waislamu kupenda amani na kukumbusha serikali kusimama katika nafasi yake ikiwemo kuonyesha ukali kwa mtu yeyote au kikundi cha watu wenye thamira mbaya ya kuvunja amani ya nchi kwa maslahi yao.
Waziri wa maji Mh Profesa Jumanne Magembe,akijibu risala aliyosomewa,ametumia nafasi hiyo kuwashauri waumini wa dini ya kiislamu kujenga tabia ya kuishi kwa amani miongoni mwao na miongoni mwa jamii kwa ujumla maana hata Quruani tukufu ya mwenyezi Mungu usisitiza sana kila mcha Mungu kuishi kwa kufuata sheria za Muumba wake ambayo suala la Amani ni muhimu sana kwa maendeleo ya familia na taifa kwa ujumla.
No comments:
Post a Comment
Newer Post
Older Post
Home
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment