Mume wa Farzana Parveen ambaeni mwanamke mjamzito wa Pakistan
aliepigwa mawe hadi kufa kutokana na kuamua kuolewa na Mwanaume
anaempenda kinyume na pendekezo la familia la kutaka aolewe na mwanaume
wanaemtaka wao, amekiri kufanya mauaji ya mke wa kwanza kabla ya Farzana
na kusema alifanya hivyo ili aweze kufunga ndoa na Parveen
Mwanaume huyo Mohammad Iqbal amesema alitaka kuwasilisha maombi yake
kwa Parveen hivyo aliamua kumuua mke wake kwanza ambapo mamlaka za
nchini Pakistan zimesema ni kweli Mwanamke huyo wa kwanza aliuwawa miaka
sita iliyopita.
Baaday a mauaji Iqbal alikamatwa na polisi na baadae kuachiwa kwa
dhamana kwasababu mtoto wake wa kiume alimsamehe kutokana na kitendo
hicho.
Mtoto
wake ambaye kwa wakati huo alikuwa na umri wa miaka 20, amethibitisha
taarifa hizo na kusema baba yake alitumikia kifungo cha mwaka mmoja
gerezani kutokana na mauji hayo.
Parveen ambae ndio mke wa pili baada ya wa kwanza kuuwawa, alikuwa na
ujauzito wa miezi mitatu na alipigwa mawe hadi kufa na kundi la watu
wakiwemo kaka zake, baba yake mzazi na ndugu wa familia yake Mashariki
mwa mji wa Lahore kwa sababu aliamua kuolewa na Mwanaume ambae familia
yake haikua inamtaka.
Tayari waziri mkuu wa Pakistan Nawaz Sharif amemtaka waziri wa Jimbo
hilo kuwasilisha maelezo juu ya tukio hilo la Mwanamke huyu kuuwawa na
ujauzito wake.
Hutaki kupitwa na stori kubwa kama hizi? niko tayari kukutumia wakati wowote iwapo utajiunga na mimi kwa kubonyeza
No comments:
Post a Comment