Jeshi
la Polisi Mkoa wa Dodoma linawashikilia watu 34 wakazi wa Mji mdogo wa
Kibaigwa Kata ya Kibaigwa Wilaya ya Kongwa Mkoa wa Dodoma kwa makosa ya
kufanya fujo na kuharibu mali tukio lililotokea tarehe 05/05/2014 majira
ya saa 13:30Hrs
.
Kamanada
wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID
MISIME – SACP amesema Vijana wanaokadiriwa kuwa zaidi ya miatatu
wakishirikiana na Wabeba mizigo wa Soko Kuu la Mazao la Kibaigwa,
walifanya maandamano bila kibali na kung’oa bango la Halmashauri ya
Wilaya ya Kongwa lenya tangazo la kutoruhusu wafanyabiashara kuingiza
mazao sokoni bila kulipa ushuru uliowekwa kwa mujibu wa sheria.
Kamanda MISIME amesema chanzo cha vurugu hizo ni wabeba mizigo wa soko la mazao kibaigwa kupinga kitendo cha Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kuweka tangazo la kutoza ushuru wa mazao sokoni hapo wakidai kwamba linawakosesha kufanya kazi zao kwani wateja wanashindwa kuingiza mazao sokoni na wao kukosa kazi.
No comments:
Post a Comment