Simplfy language

thanx

Wednesday, April 9, 2014

NGASSA AONYESHA UPENDO KWA WEMA SEPETU...

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
NGASSA: “Diamond ni rafiki yangu, lakini mpira huu nitampelekea Wema kwa kuwa ni shemeji yangu na tunaheshimiana sana,” alisema Ngassa na kuongeza: Mrisho Ngassa wa Yanga, jana alifanikiwa kufunga mabao matatu ‘hat trick’ katika mechi dhidi ya JKT Ruvu, lakini ametoa kali kwa kusema kuwa mpira aliokabidhiwa kwa kufunga mabao hayo, anaupeleka kwa shemeji yake, Wema Sepetu. Akizungumza baada
Wema Sepetu ‘Madam’.
ya mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara iliyomalizika kwa timu yake kupata ushindi wa mabao 5-1, Ngassa huku akionyesha kuwa na furaha, alisema kuwa mpira huo umeongeza hamasa kwa timu yake, lakini moja kwa moja atampelekea Wema ambaye ni mpenzi wa mwanamuziki Diamond. “Mashabiki hawatakiwi kukata tamaa na timu yetu, sisi tutapigana mpaka dakika ya mwisho ili kuhakikisha tunashinda mechi zote. Wakati mwingine tunashindwa kucheza vizuri mikoani kwa kuwa viwanja vinakuwa havina ubora mzuri.” Yanga imepata ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya JKT Ruvu na hivyo kuamsha mbio za ubingwa dhidi ya Azam ambao ndiyo vinara wa Ligi Kuu Bara, lakini kipa Juma Kaseja na mshambuliaji raia wa Uganda, Emmanuel Okwi hawakuwepo kwenye kikosi kilichoanza wala kwenye benchi. -

No comments:

Post a Comment