NGASSA: “Diamond ni rafiki yangu, lakini mpira huu nitampelekea 
Wema kwa kuwa ni shemeji yangu na tunaheshimiana sana,” alisema Ngassa 
na kuongeza: Mrisho Ngassa wa Yanga, jana alifanikiwa kufunga mabao 
matatu ‘hat trick’ katika mechi dhidi ya JKT Ruvu, lakini ametoa kali 
kwa kusema kuwa mpira aliokabidhiwa kwa kufunga mabao hayo, anaupeleka 
kwa shemeji yake, Wema Sepetu. Akizungumza baada  
ya mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara 
iliyomalizika kwa timu yake kupata ushindi wa mabao 5-1, Ngassa huku 
akionyesha kuwa na furaha, alisema kuwa mpira huo umeongeza hamasa kwa 
timu yake, lakini moja kwa moja atampelekea Wema ambaye ni mpenzi wa 
mwanamuziki Diamond. “Mashabiki hawatakiwi kukata tamaa na timu yetu, 
sisi tutapigana mpaka dakika ya mwisho ili kuhakikisha tunashinda mechi 
zote. Wakati mwingine tunashindwa kucheza vizuri mikoani kwa kuwa 
viwanja vinakuwa havina ubora mzuri.” Yanga imepata ushindi wa mabao 5-1
 dhidi ya JKT Ruvu na hivyo kuamsha mbio za ubingwa dhidi ya Azam ambao 
ndiyo vinara wa Ligi Kuu Bara, lakini kipa Juma Kaseja na mshambuliaji 
raia wa Uganda, Emmanuel Okwi hawakuwepo kwenye kikosi kilichoanza wala 
kwenye benchi. -
 
No comments:
Post a Comment