Pages
Home
Kitaifa
Kimataifa
Michezo
Burudani
Makala
Usilolijua
Leo katika historia
Picha
Teknolojia
Afya
Simplfy language
thanx
Sunday, September 1, 2013
Mwanamke ateuliwa waziri mkuu Senegal
Mwanamke ateuliwa waziri mkuu Senegal
Rais Macky Sall wa Senegal amemteua mwanamke kuwa waziri mkuu mpya, masaa tu baada ya kumtoa kazini mwanasiasa aliyemteua aliposhika madaraka mwaka jana.
Aminata Touré, waziri wa zamani wa sheria, aliiambia redio ya taifa kwamba amekubali amri ya rais ya kuunda serikali mpya.
Bwana Mbaye, aliyewahi kufanya kazi kwenye benki, hakuwa mfuasi wa chama chochote cha kisiasa.Haikutolewa sababu ya Bwana Adbou Mbaye kutolewa kazini.
Bi Touré atakuwa mwanamke wa pili kuwa waziri mkuu nchini Senegal - baada ya Madior Boye, aliyeshika wadhifa huo kwa miezi 18 mwaka wa 2001.
Bwana Sall alimshinda Rais Abdoulaye Wade katika uchaguzi wa rais wa March 2012, akiahidi kupambana na umaskini na rushwa. )
No comments:
Post a Comment
Newer Post
Older Post
Home
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment