MSANII wa filamu Bongo, Mayasa Mrisho ‘Maya’ amewataka wasanii wenzake kusameheana na kupendana kwani kifo cha msanii mwenzao, Sheila Haule ‘Recho’ kimempa fundisho kubwa.
Akizungumza na paparazi wetu, Maya alisema vifo vya wasanii vinavyotokea kila kukicha vinaumiza na kusikitisha hivyo wasanii wanatakiwa kusameheana pale walipokoseana na kupendana kwani kifo kipo wakati wowote.
“Inahuzunisha hata mwezi haujapita tumeshawapoteza wasanii wawili tunatakiwa kumuomba Mungu sana na wale wasanii wenye mabifu wapatane, upendo utawale kati yetu kwani hatujui tunakufa lini,”alisema Maya.
No comments:
Post a Comment